NDOTO NA MAANA ZAKE

1610538,DirectLink_1,22607892,https://www.profitablegatecpm.com/cmsm44evgd?key=14968b76cc3b7bd087c4ee0b9793b1a0
NDOTO
Ndoto ni nini?
          NDOTO ni mfululizo wa picha, mawazomihemko na hisia ambao hutokea akilini, kwa kawaida bila makusudi, katika hatua fulanifulani za usingizi.[1]
Yaliyomo na malengo ya ndoto hayajaeleweka vizuri, ingawa tangu zamani yamejadiliwa sana katika sayansi (hasa elimunafsia) na katika diniFani inayochunguza ndoto kisayansi inaitwa onirolojia.[2]
Kwa kiasi kikubwa ndoto zinatokea wakati usingizini macho yanapogeukageuka zaidi, ambapo utendaji wa akili ni mkubwa karibu sawa na mtu anapokuwa macho. Zikitokea wakati mwingine wa usingizi, ndoto hazikumbukwi sana baada ya kuzinduka.[3]
Muda wa ndoto unaweza kuwa tofauti sana: tangu sekunde chache hadi dakika 20–30.[3]
Kwa wastani watu wanapata ndoto 3 hadi 5 kwa usiku, wengine hadi 7;[4] lakini nyingi zinasahaulika mara au mapema.[5] Watu wanaweza kukumbuka zaidi ndoto zao wakiamshwa wakati wa usingizi wa macho kugeukageuka.
Ndoto zinaelekea kudumu zaidi kadiri muda wa usiku unavyozidi kwenda.[6]
Ndoto zinaweza kuwa za aina mbalimbali: nje za uwezekano katika maisha ya kawaida, za ajabuajabu, za kutisha, za kusisimua, za kishirikina, za kidini, za kusikitisha, za kijinsia, n.k. Zinaweza pia kumsaidia msanii kubuni kitu.[7]
Kwa kawaida ziko nje ya udhibiti wa mtu, isipokuwa mtu anapoota akiwa anajitambua (ndoto za mchana).[8]
Rai kuhusu maana ya ndoto zimetofautiana sana kadiri ya nyakati na utamaduni.[9]
Kumbukumbu za zamani zaidi kuhusu ndoto ni za miaka 5000 hivi iliyopita huko Mesopotamia, ambapo zilichorwa katika vigae.
Katika Ugiriki wa Kale na Roma ya Kale, watu walisadiki ndoto zinaleta ujumbe kutoka kwa mungu fulani au marehemu fulani na kwamba zinatabiri ya kesho.
NDOTO KI BIBLIA;
Image result for ndoto ni nini kibiblia  Katika Biblia, ndoto zilizotoka kwa Mungu sikuzote zilikuwa na kusudi hususa. Ni kweli kwamba nyakati nyingine mwenye kupokea ndoto hakuelewa mara moja maana ya ndoto hiyo. Hata hivyo, katika visa vingi ‘Afunuaye siri’ mwenyewe alitoa ufafanuzi ili kusiwe na mashaka yoyote juu ya maana ya ndoto. (Danieli 2:28, 29;Amosi 3:7) Ndoto zilizotoka kwa Mungu hazikuwa zenye maana isiyo dhahiri kama vile ndoto za kawaida.
Mara kwa mara, Mungu alitumia ndoto kuwalinda watu waliohusika kwa njia kubwa katika utimizo wa kusudi lake. Si watumishi wa Mungu tu waliopokea ndoto hizo. Kwa mfano, wanajimu waliotembelea mtoto Yesu hawakurudi kwa Herode, aliyetaka kumwua Yesu kama alivyokuwa amewaomba. Kwa nini? Walipokea onyo katika ndoto. (Mathayo 2:7-12) Jambo hilo lilimpa Yosefu,fursa ya kukimbia Misri pamoja na jamaa yake, kwa kufuata mwelekezo ambao hata yeye alikuwa amepokea katika ndoto. Hilo liliokoa maisha ya mtoto Yesu.—Mathayo 2:13-15.
Karne nyingi mapema,Mfalme mmoja wa Misri aliota ndoto kuhusu masuke saba manene yaliyolinganishwa na masuke saba dhaifu, na ng’ombe saba wanono waliolinganishwa na ng’ombe saba waliokonda. Mungu alimsaidia Yusufu kufasiri ndoto hizo kwa usahihi: Miaka saba ya shibe nchini Misri ingefuatwa na miaka saba ya njaa. Kujua mapema jambo hilo kuliwapa Wamisri fursa ya kutayarisha chakula na kukiweka akiba. Hiyo ilikuwa njia ya Mungu ya kuhifadhi wazao wa Abrahamu na kuwapeleka Misri.—Mwanzo, sura ya 41; 45:5-8.
Mfalme Nebukadneza wa Babiloni pia aliota ndoto. Ndoto hiyo ilitabiri kutokea na kuanguka kwa tawala za ulimwengu za wakati ujao, ambazo zingeathiri moja kwa moja watu wa Mungu. (Danieli 2:31-43) Baadaye aliota ndoto nyingine iliyotabiri kichaa na kupona kwake. Ndoto hiyo ya kiunabii ilikuwa na utimizo mkubwa zaidi, ilionyesha kimbele kusimamishwa kwa Ufalme wa Kimesiya, ambao ungetumiwa na Mungu kutimiza mapenzi yake.—Danieli 4:10-37.

MAWASILIANO KATIKA NDOTO.
Image result for ndoto ni nini kibiblia                Hatahivyo bado Mungu aliwasiliana na baadhi ya watu kwa njia ya ndoto. Lakini Biblia huonyesha kwamba matukio hayo yalikuwa machache sana. Mungu hakuwasiliana kupitia ndoto kwa ukawaida. Watumishi wengi waaminifu wa Mungu hawakupokea kamwe ujumbe kutoka kwa Mungu kwa njia ya ndoto. Mawasiliano kati ya Mungu na wanadamu kwa njia ya ndoto yanaweza kulinganishwa na kutenganishwa kwa maji ya Bahari Nyekundu. Ingawa alifanya hivyo mara moja, tunajua kwamba hiyo si njia yake ya kawaida ya kushughulika na watu wake.—Kutoka 14:21.
Mtume Paulo alitambua kwamba katika siku zake Mungu alitumia roho yake kuwapa watumishi wake vipawa vingi vya ajabu. Paulo alisema hivi: “Mmoja hupewa usemi wa hekima kupitia ile roho, mwingine usemi wa ujuzi kulingana na roho ileile, mwingine imani kwa roho ileile, mwingine zawadi za maponyo kwa roho moja hiyo, mwingine bado utendaji wa kazi zenye nguvu, mwingine kutoa unabii, mwingine ufahamu wa matamko yaliyopuliziwa, mwingine lugha tofauti, na mwingine fasiri ya lugha.” (1 Wakorintho 12:8-10) Ijapokuwa ndoto kutoka kwa Mungu hazitajwi mahususi, ni wazi kwamba ndoto kutoka kwa Mungu zilikuwa mojawapo ya zawadi za roho ambazo zilitabiriwa katika Yoeli 2:28 ambazo Wakristo kadhaa walipokea.—Matendo 16:9, 10.
Hata hivyo, mtume huyo alisema kuhusu vipawa hivyo vya kipekee: “Kama kuna zawadi za kutoa unabii, zitaondolewa mbali; kama kuna lugha, zitaacha kuwako; kama kuna ujuzi, utaondolewa mbali.” (1 Wakorintho 13:8) Ni dhahiri kwamba zawadi ambazo “zingeondolewa mbali” zilitia ndani njia mbalimbali za mawasiliano kutoka kwa Mungu. Baada ya kifo cha mitume, Mungu hakuwapa tena watumishi wake vipawa hivyo vya kipekee.
Image result for ndoto ni nini kibibliaLeo, wataalamu bado wanajaribu kuelewa mambo yote yanayohusiana na kuota ndoto na ikiwa hunufaisha kwa njia yoyote. Biblia haina maelezo yoyote kuhusu manufaa ya kuota ndoto. Hata hivyo, kuna onyo katika Biblia kwa wale wanaosisitiza kwamba ndoto zao ni mawasiliano kutoka kwa Mungu. Andiko la Zekaria 10:2lasema hivi: “Waaguzi, . . . wameleta habari za ndoto za uongo.” Mungu huonya pia dhidi ya kubashiri. (Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Kwa kufikiria maonyo hayo, siku hizi Wakristo hawatarajii kupokea mwongozo wa kimungu katika ndoto zao. Badala yake, wanaona ndoto kuwa hali inayotukia usingizini tu.

                                                                                                            

HIZI NI BAADHI YA NDOTO WANAZOOTA SANA WANADAMU NA SHETANI HUFANYA SANA MASHAMBULIZI KUPITIA AINA HII YA NDOTO

NDOTO 0001; Wakati nimelala usiku, mara nikaota nnasikia mlio wa bunduki (risasi) na nikapata shida sana ila ndoto halisi siikumbuki nnaomba msaada kujua uhalisia wa ndoto hii kwamaana nnatambua ndoto ni uhalisia.
               MAJIBU; Tambua yakwamba uko katika mapambano, Jua yakwamba shetani muda wate yuko kazini kupitia mawakala wake kama wachawi/majini...nk, hivyo mara nyingi/zote shetani hutumia mlio wa bunduki au kukupiga risasi katika ndoto na ukajua ni ndoto TU! la! hasha si ndotoTU!. Hiyo inamaanisha mawakala wa shetani anapigana na wewe kupitia mtu anaekufahamu vema sana, Bunduki ikielekezwa kwako, humaanisha shamulizi la moja kwa moja kutoka kwa wachawi. Lakini taarifa au kusikia mlio wa risasi katika ndoto ni shambulizi la kichawi dhidi ya mpendwa wako na sio wewe mwenyewe. HATA HIVYO mlio wa risasi katika ndoto huashilia KIFO kutoka roho za maajenti wa kichawi au wachawi wenyewe.
              SULUHISHO; Endapo umeota ndoto ya namna hii haraka sana AMKA kama umeshtuka usingizini na kisha anza kuomba kinyume na roho za adui, na hakuna nguvu nyingne yoyote inayoweza kushinda vita hivyo ispokua NGUVU YA JINA LA YESU PEKEE, omba ukilitaka jina la bwana yesu kuingilia kati vita dhidi ya wachawi hao na nguvu zote zilizo kinyume nawewe, na pia ili kushinda kirahisi unapaswa kuingia katika mfungo wa maombi hata kama ni ya masaa kuminambili (masaa 12) ili kushinda vita hiyo maana mlio wa risasi katika ndoto humaanisha tukio ambalo liko jirani kabisa kutekelezwa hivyo linakuhitaji kupambana kwa haraka sana. (Inakupasa uwe ndani ya kristo yaani uwe umeokoka maana huwez hushinda hiyo vita nje ya BWANA YESU KRISTO TU! kiri uweza wa DAMU YA YESU KRISTO, kabla na baada ya ushindi kupitia maombi unayoomba!.

NDOTO 0002;Mtu mmoja akasema ameota ndoto anakula samaki wabichi ndotoni! akapagawa sana na kupata shauku ya hali ya juu kutaka kutambua ni nini maanayake ndoto hii.

        MAJIBU;Mara tu utakapoona katika njozi unakula samaki wabichi, uwe na uhakika maanayake ni kwamba maadui zako wanapigana na wanakulana wenyewe kwa wenyewe.

        SULUHISHO; Hapo MUNGU anakujulisha moja kwa moja kwamba vita umekwisha ishinda hivyo kuuimarisha ushindi haraka sana unatakiwa kumshukuru mungu na kuingia kwenye maombi ambayo utamtukuza MUNGU kwa vuwango vikubwa pia usisahau kujiwekea ulinzi mwingi wa DAMU NA JINA LA YESU KRISTO. (mathayo 18:18)

NDOTO 0003; Mara katika ndoto ukiota unachana karatasi/makaratasi, tena inawezekana mtumwingne anachana karatasi mbeleyako, yaweza kua mwenyewe binafsi unachana au mtu wa karibuyako Je! yaweza kua ni nini maanayake?

        MAJIBU;Naam ukiona/ukiota jambo hili katika njozi za usingizi wako uwe na uhakika kua mashtakayako/kesi yako hukumu yako imefutwa/ imechanwa mojakwamoja yaani hakuna tena hukumu juu yako.

        SULUHISHO;Katika hali hiyo huo ni ushindi mkubwa sana unapaswa kumshukuru mungu na kuuimarisha ushindi huo kimaombi zaidi na zaidi. (wafilipi 2:10)


 NDOTO YA DARASANI AU KUFANYA MTIHANI
 
Moja ya ndoto ambayo watu wengi wameuliza ni ndoto ya kuota upo darasani unafanya mtihani, unatakiwa kufanya mtihani, na zingine kama hizo.
 
Ndoto hizi zinahusiana na UHITAJI WA MAARIFA. Shule ni eneo ambalo unasoma ili upate MAARIFA ya kuweza kukusaidia kuvuka kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine iliyo BORA ZAIDI.
 
Nimeweka msisitizo iliyo “bora zaidi” kwani Shule ambayo haibadilishi maisha yako haina msaada kwako. Hivyo tunaposoma, tunapata maarifa na tunatumia maarifa tuliyopata shuleni ili kuishi kwa kiwango bora zaidi.c
 
Daniel 1:3—4 “Mfalme akamwambia Ashpenazi, mkuu wa matowashi wake, awalete baadhi ya wana wa Israel, na uzao wa kifalme, na wa uzao wa kiungwana; vijana wasio mawaa, wazuri wa uso, wajuzi wenye hekima, WEREVU KWA SABABU YA MAARIFA YAO, wenye kufahamu elimu, watakaoweza kusimama katika jumba la mfalme; tena alimwambia awafundishe elimu ya wakaldayo, na lugha yao.”
 
Ukiendelea kusoma utaona Daniel na wenzake walikuwa miongoni mwa vijana hao. Nilitaka uone kipengele kinachosema “werevu kwa sababu ya maarifa yao.” 

“Basi, kwa habari za hao vijana wanne, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekima; Daniel naye alikuwa na ufahamu katika maono yote, na ndoto” (Daniel 1:17).
 
Kwa hiyo ndoto unayoota upo Shuleni tafsiri yake ni uhitaji wa maarifa fulani ambayo yanatakiwa yakutoe sehemu moja na kukupeleka sehemu nyingine bora zaidi.
 
KUMBUKA HII: Adui wa kwanza wa mafanikio katika maisha yako SIYO Shetani bali UKOSEFU WA MAARIFA. “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa” (Hosea 4:6a). Kwa hiyo, ukiona umekwama katika eneo fulani la maisha, huhitaji tu maombi ila UNAHITAJI MAARIFA.
 
“Katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Daniel, kwa sababu ya kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la BWANA lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalem nabii, yaani miaka sabini. Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu” (Daniel 9:2—3).

Kwa hiyo Daniel, kwa kusoma vita alipata maarifa fulani ndipo akaingia kuomba. Mungu alimtuma malaika Gabriel naye akasema na Daniel kama maandiko yanavyotuambia: “Akaniagiza, akaongea nami, akasema, Ee Danieli, nimetokea sasa, ili nikupe akili upate kufahamu” (Daniel 9:21.)
 
Kwa hiyo Daniel alihitaji MAARIFA. Vivyo hivyo, unapoota upo Shuleni, unahitaji maarifa. Unatakiwa uombe Mungu akupe maarifa unayohitaji. 

Mashuleni, kinachotumika kukupima kama umepata maarifa unayotakiwa kuyapata ni MTIHANI. Kuna kufeli mtihani kwa aina tofauti. Tuangalie chache:
 
KUFELI MTIHANI: Katika ulimwengu wa mwili, mtu anapofeli mtihani maana yake hajapata maarifa anayotakiwa kuyapata ili aweze kufaulu. Katika ulimwengu wa roho ni vivyo hivyo. Unapofeli mtihani maana yake kuna maarifa ambayo unatakiwa uwe nao lakini hauna. 

Kwa sababu hiyo, ukosefu wa maarifa hayo umekukwamisha katika eneo fulani. Inaweza kuwa katika uchumi, biashara, kiroho, au eneo lingine.
 
KUFELI KWA SABABU YA KUCHELEWA MTIHANI: 

A. Kufeli kwa kuchelewa tu: Mtu mwingine anafeli mtihani kwa sababu alichelewa ila majibu ya mtihani anayajua. Ukiona unachelewa kwenye chumba cha mtihani lakini maswali unayajua, na unajikuta umefeli kwa kutokuwa na muda, maana yake MAFANIKIO YAKO YAMEFUNGWA NA MUDA. 

Moja ya silaha ambazo Shetani anazitumia kukwamisha mafanikio ya watu ni MAJIRA/NYAKATI. “Naye atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na Sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati” (Daniel 7:25). 

Kama mafanikio yako yamefungwa kwenye muda, shida siyo kutokuwa na maarifa. Ndio maana unaingia kwenye mtihani, maswali unaweza kuyajibu, lakini muda hautoshi. Maarifa unayo ila adui ameteka muda wako ili usitimize kusudi unalotakiwa kutimiza kwa wakati ulioamuriwa. Kumbuke “Kwa kila jambo kuna majira yake” (Mhubiri 3:1). 

Hivyo unachotakiwa ni kuukomboa wakati wako ili maarifa uliyonayo uyatumie kutimiza kusudi la Mungu kwa wakati sahihi. “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama wenye hekima; mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu” (Waefeso 5:15—16). 

B. Kufeli kwa kuchelewa na kutokujua: Mwingine anafeli mtihani kwa sababu pamoja na kwamba amechelewa lakini pia hajui cha kuandika. Maana yake huyu mtu hata kama angewahi kuingia kwenye mtihani angefeli. 

Ndoto ya namna hii maana yake shida haipo tu kwenye muda bali na maarifa pia. 

KUANGALIZIA KWENYE MTIHANI: Mtu mwingine anaota yupo anaangalizia mtihani kwa mwenzake. Maana yake unataka kutumia maarifa ya mwingine ili ufaulu. 

Ndoto ya namna hii maana yake kuna mambo unataka kuyafanya katika maisha yako au unayafanya kwa sababu unaiga lakini sicho Mungu alichokikusudia. 

Hii ilimkuta Isaka ambaye njaa ilipotokea katika nchi yake, alitaka kwenda Misri kwani watu walikuwa wanaenda Misri kufuata chakula. “BWANA akamtokea, akasema, Usishuke kwenda Misri, kaa katika nchi nitakayokuambia” (Mwanzo 26:2). 

Hivyo ukiota unaangalizia kwenye mtihani, muombe Mungu akuambia kile ambacho anataka ufanye wewe kama wewe.
 
KURUDISHWA DARASA AMBALO UMESHAVUKA
 
Katika ulimwengu wa roho, kiwango cha maarifa hakipimwi na elimu mtu aliyonayo bali katika kufikiri. Neno linasema “anonavyo nafsini mwake ndivyo alivyo” (Methali 23:7).
 
Mtu anapoota ndoto yupo darasa ambalo ameshavuka kwa jinsi ya mwili maana yake kufikiri kwa mtu huyo kuko chini ya kiwango Mungu anachotegemea. Kwa mfano: mtu ameshamaliza chuo kikuu lakini kila mara anaota yuko shule ya msingi.
 
Maana yake kiwango cha kufikiri cha mtu huyo ni cha awali. Kinachotoa kiwango cha maarifa ni kiwango cha neno la Mungu linilopo ndani ya mtu. Kwa mfano: kuna watu wengine miaka yote hawakui kiroho na miaka yote wanajadili mambo ya kidini badala ya mambo ya ufalme wa Mungu.
 
“Kwa maana, iwapasavyo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu” (Waebrania 5:12). 

Baada ya muda fulani, Mungu anategemea tukue katika kulijua neno lake ili tufikiri kwa kiwango cha juu zaidi. Mungu anategemea tuache mafundisho ya kwanza na kuwa na maarifa zaidi ili tuweze kufanya maamuzi sahihi juu ya maisha yetu (Waebrania 6:1; Waebrania 5:14).
 
Unaweza kuwa unafanya biashara au shughuli fulani na shughuli hiyo haikui kabisa. Moja ya sababu inaweza kuwa wewe kushindwa kupanua wigo wa kufikiri ili uweze kwenda hatua iliyo bora zaidi. Kwa hiyo Mungu anaweza kukuletea ndoto uko shule ya msingi wakati ulishamaliza chuo na labda una familia yako.
 
Unapoota ndoto za darasa ambalo ulishavuka muda mrefu maana yake umekwama katika kufikiri. Mtu anaweza kukwama kufikiri kwa sababu nyingi lakini pia Shetani anaweza kukamata fikra ya mtu.
 
Vita ya kwenye fikra huwa inapiganiwa kwenye elimu. Kuna elimu ambayo adui atapambana usiipate kwani hataki upate maarifa fulani. 

“Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na kuteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo” (2 Wakorintho 10:3—5).
 
Umewahi kujiuliza kwa nini watu wengi hawapokei elimu ya ufalme wa mbinguni wakati Yesu anasema utafuteni kwanza ufalme wa Mungu” (Matayo 6:33)
<!-- Google Tag Manager -->
<script>(function(w,d,s,l,i){w[l]=w[l]||[];w[l].push({'gtm.start':
new Date().getTime(),event:'gtm.js'});var f=d.getElementsByTagName(s)[0],
j=d.createElement(s),dl=l!='dataLayer'?'&l='+l:'';j.async=true;j.src=
'https://www.googletagmanager.com/gtm.js?id='+i+dl;f.parentNode.insertBefore(j,f);
})(window,document,'script','dataLayer','GTM-T7RRGW4F');</script>
<!-- End Google Tag Manager -->

Comments

  1. kwamfano ukiota unavalishwa pete ya uchumba mchana

    ReplyDelete
    Replies
    1. Minategemea na hali ya ndoto hiyo mpaka kuijua. ila yaweza kua baraka ambayo imekaribia pia kunahitaj taadhdari kubwa mnoooo

      Delete
  2. Nimeota ndoto moja ambayo siielewi na kila saa inanijia.
    Nimeota nipo shule Nasoma postgraduate safari hii nilioota Nasoma nao ni watu tofauti kabisa na niliokuwa nasoma nao, na mwalimu wetu ni Raisi Magufuli na topic alifundisha inaitwa Curriculum Sasa mie nikachelewa sijui Wapi nikakuta tayari ameshatoka Ila kuna notice zimeachwa watu wanacopy na kwenye Hizo notice kuna kuchora ramani ya Dunia, nikawa natoa macho pale maana kuchora ramani nimechoka secondary sijui itakuwaje, Ila pia nikawa nawaambia wale wanafunzi wenzangu ni watu Wazima kabisa kuwa hii topic nimeiota Hivi hivi kuwa ticha anaifundisha. Then nikastuka

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hongera BWANA YESU anakuonyesha njia. Kwanza anahitaji umsikie kama mwalimu na pili amekufungulia mlango mkubwa hivyo nijuhudizako kunyenyekea katika maombi ilikwamba akuonyeshe kusudi maalumu na ndiomaana hukuwahi kipindi darasani inamaanisha unahitajika kumtafuta zaidi mwalimu (BWANA YESU KRISTO) yako mambo kwaajili along anayo anampango wakukupa channel ya maono yako.

      Delete
  3. Leo tena nikaota ingine.
    Ndugu zangu upande WA baba angu wamekuja wengi kwangu kuna harusi ya mdogo etu ambae tayari ameshafunga ndoa. Wapo hapo tunajiyayarisha kwenda harusini. Nikastuka nikastuka nikarudi tena kulala nikaendelea kuota Tupo ukumbini now tunataka kuingia

    ReplyDelete
    Replies
    1. Nimuendelezo wa ndoto ya awali, inamaanisha kama utakua nje na utaratibu ambao Mungu ameukusudia kwako yako mambo mabaya yatakayojiinua zaidi kwako ili kuhakikisha umedhoofika kiroho na kiuchumi kabisa. Si mafanikio sherehe hiyo ni vita...., (rejea nlichokwambia katika ndoto ulioota Kwanza nn ufanye) NI MUNGU TU, Upo kwenye channel ya Mungu usitoke.

      Delete
  4. Nikaota tena Nina mtoto nanyonyesha, na ingine Tupo kwa harusi tena though sio ya ndugu niko Marafiki tu wengine

    ReplyDelete
    Replies
    1. BWANA YESU ANAKUPENDA SANAAA ZOTE HIZI NI MSISITIZO WA NDOTO YA AWALI. kasome Ayubu 33:15

      Delete
    2. Siku hizi kuna ndoa zinafungwa katika ndoto hasa ndoa za majini paki jini likipenda kuangusha Imani ako na wengine uota wakiwa na mimba na kuzaa lakini pia huanza kunyonyeshs kwenye ndoto kwo omba Sana yawezekana upo katika maagsno ns nguvu za giza ns pengine umezaa nao

      Delete
  5. Mume wangu leo kaota ndoto ya ajabu mie nastuka napigwa mateke 😳 Wee mbona wanirushia mateke anastuka ananiambia nimeota ndoto mbaya kweli🙆🏾, Ameota Yuko Nairobi na rafiki yake wakawa wameenda kutembelea maduka ya Kaja WA huyo rafiki yake Sasa huyo rafiki yake na Kaka zake wote ni wachezaji mpira wakamwambia yeye ili asiboreke wakampa godoro akae Ila anashangaa hajui ilikuwaje lile godoro likawa kama linaelea hewani akatokea mbwa mweusi anataka kumng'ata akamfukuza akaja mbwa mwengine mwekundu akawa nae anataka kumng'ata ndio huyo Sasa akawa anammrushia mateke kumbe narushiwa mie live😅

    ReplyDelete
    Replies
    1. Bwana YESU anaipenda familiayako anawakumbusha hasa mume, kuwa karibu na familia zaidikuliko watu wakaribuyenu. Kwamba kupewa nafasi yakutoboreka na wanafamilia ugenini-ni-ku sahau kwamba anafamilia inayomuhitaji saa zote, na mbwa hao ni uovu ambao kama hataingia katika kumtafuta Mungu ili kuiponya familia yake uovu huo utaiingilia familia kupitia mke. Hivyo wote mnalo jukumu la dhati tena lenye maana kuingia katika maombi kwaajili ya hili. ( mjitahidi walau maombi kwa siku tatu kuiponya familia) BWANA YESU AWABARIKI NAMI NINAWAOMBEA NINYI ILI KRISTO AWASHINDIE.

      Delete
  6. Na je ukiota ndoto unaokota hela za vimia mia inamaanisha nn

    ReplyDelete
  7. MUNGU ANATAKA KUKUBARIKI KUANZIA MAHALA ULIPO, ILA UNADHARAU HALI ULIONAYO. MUNGU HUANZIA HAPO ULIPO IKUBALI HALIYAKO NA TENA TAZAMA KWAUMAKINI KWAKUITUNZA AMANA YAKO INAYOKUPA KIPATO MAANA MUNGU ANAKUHIMIZA KATIKA UAMINIFU ILI AKUNYANYUE ZAIDI.

    ReplyDelete
  8. Habari kuota unaokota coins za Mia, Mia mbili na Mia tano Ina maana gani, na pia kuota unachuma maembe juu ya mti wa maembe

    ReplyDelete
    Replies
    1. Rejea nilivyo mjibu mwenye swali la juu yako katika comment hizi.

      Delete
    2. MUNGU ANATAKA KUKUBARIKI KUANZIA MAHALA ULIPO, ILA UNADHARAU HALI ULIONAYO. MUNGU HUANZIA HAPO ULIPO IKUBALI HALIYAKO NA TENA TAZAMA KWAUMAKINI KWAKUITUNZA AMANA YAKO INAYOKUPA KIPATO MAANA MUNGU ANAKUHIMIZA KATIKA UAMINIFU ILI AKUNYANYUE ZAIDI.

      Lakini pia kuhusu kuchuma embe yaani unamuhitaji mingu akusaidie katika kufanikiwa kwako ila umekua ukiwaza na kuharakia, hivyo Mungu anakukumbusha katika ndoto kwamba anakukumbusha na hajakusahau punguza uharaka wakutamani mafanikio itakugharimu yeye amekuona MUNGU WA ISRAEL anakujua kufanikiwa kwako zidi sana kumtafuta matokeo yako yako karibu.

      Delete
  9. Bwana yesu asifiwe ukiota unasoma na watu ambao ulishasoma nao awali na walikua wanaakil, ww ukaota unasoma nao tena wakati kila mtu kwa sasa anasoma chuo chake hlf upo nao darasa moja ila hujui n sehemu gan

    ReplyDelete
  10. Bwana Yesu asifiwe ..huwa namuota sana mmewangu kwa mabaya..nimeshamuota akiwa na mwanamke mwingine kama mara tatu hivi..dhen nikamuota amerudi nyumbani na mwanamke mwingine wakiwa wamelewa sana

    ReplyDelete
    Replies
    1. Habari ya uzima. Hii nikwahabari ya matengenezo familia yenu inahitaji matengenezo wasiliana nami kwa kusaidiana pia hata kimaombi na kimaombezi. Pia kuna maelezo zaid nnahitaji kufahamu.

      Delete
  11. Pia nimeshaota sana nikiwa chuoni nafanya mtihani wa mwisho nimechelewa kuingia chumba cha mtihani sijui mana yake nn jmn

    ReplyDelete
  12. Huwa nikiwa katika toba ya uzinzi huwa naota Mara nyingi nikiwa na mwanaume chumbani,au naingia logde,au tunajiandaa kufanya hcho kitendo ..kama Leo nimeota tupo chumbani ananiforce huku Mimi namkemea mpaka akaacha naomba msaada tafadhali

    ReplyDelete
    Replies
    1. BWANA YESU AKUSAIDIE SANA....
      KWAKU KWA YESU HAKUNA GUMU YOOOTE YANAWEZEKANA HILI NI DOGO, IKIWA UKOTAYARI KWAAJILI YA KRISTO.
      Mimi Ni mtumishi wa kristo ninazo kanuni kwaajili ya uzima wa roho na niko tayari kukupatia ili ushinde majaribu.
      Wewe upo Kama walivyo wengi hasa mabinti. Chakufanya nikuuchukia mwili kwakumpenda kristo yaani kujitoa dhabihu kwa kristo
      Mathayo : Mlango 16
      24 Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.
      Sasa Suluhisho nikwamba ufanye kwa uaminifu haya nitakayokuambia saa hii...

      Delete
    2. UNAPASWA kua na mnyororo wa maombi Mara mbili kila wiki, pili punguza au acha ubize wa mawasiliano na vijana wenye maneno ya mizaha kwamaana neno la Mungu lasema....1 Wakoritho : Mlango 15
      33 Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.
      Pia wasiliana nami kwa WhatsApp +255786620305

      Delete
  13. Bwana yesu asifiwe,nmeota ndoto napigana na kichaa...nikamshinda nikachukua fimbo aliyokua kashika nikampiga nayo nikafanikiwa kumpiga..pembeni walikuepo watu wanacheza karata hawakunisaidia walibaki wanamtizama baada ya kumshinda kichaa nikaanza kuwafokea kwa nn hawakunisaidia maana nilikua nmebeba mtoto...inaweza kuwa na maana gani

    ReplyDelete
    Replies
    1. BWANA YESU ASIFIWE SANA. pole sana kwa ndoto mbaya. Lakini nnataka kukwambia aduizako wanachezea kichapo fimbo maana yake Ni mamlaka juu yao hawana uwezo juuyako. Pia kichaa inamaana yapo mambo unayakasirikia lakini hujapata majibu kwaakilizako na unaona yanakutesa sasa MUNGU anakufumbua macho anakueleza kua hayo yote amekuweka juu yake ili uoite kwa hayo, na hao wacheza karata inamaana hutakiwi mtazama yeyote wakaribu yako MUNGU anataka ajitwalie utukufu yy binafsi KUPITIA ww. Mambo haya ni muhimu kufanya

      Delete
    2. KWAKUA NI MAFANIKIO YAKO KIROHO NA KIMWILI. UNATAKIWA UFUNGE KWAKUUGUA NA KUKEMEA SANA ROHO ZA UPINZANI THEN MWAMBIE MUNGU AKUPE DIRA YAKUPITA KATIKATI YA HAYO YOTE USIPUUZE MUNGU ANATAKA KUKUINUA SANA.Marko : Mlango 12
      36 Daudi mwenyewe alisema, kwa uweza wa Roho Mtakatifu,Bwana alimwambia Bwana wangu,Uketi mkono wangu wa kuume,Hata niwawekapo adui zakoKuwa chini ya miguu yako.

      Delete
  14. Leo ndugu yngu kanipigia simu asubuhi hii anataka kujua halii yangu ananiuliza kam kuna usalama maan ameota kuwa me nimegongwa na gar na nikafa hapo hapo kwenye ajari sasa nataka kujua je hii ndo inamaana gan??

    ReplyDelete
    Replies
    1. BWANA YESU ASIFIWE SANA. POLE KWA MSHTUKO NA BWANA AKUTIE NGUVU. KWA HILI NIKWAMBA SHETANI ANAHANGAIKA KUTAFUTA MPENYO JUU YA KUKUANGAMIZA KWA STAILI UTAKAYOONA NA KUDHANIKUA NI MABADIRIKO YA GHAFLA KIMAISHA (eidha kiuchumi, au kufungika kwa mkondowako mdogo wakujikimu na maranyingine akishindwa happy nikutaka KUKUANGAMIZA kabisa wewe au Yule aliye karibu yako sana nana hatua yake ya kufanikiwa) CHAKUFANYA ZIKO HATUA TATU MUHIMU SANA

      Delete
    2. MOJA> Kama hujamjua YESU KRISTO UNATAKIWA KUMJUA KWANZA YAANI KUMWAMINI NA KUOKOKA
      PILI>Fanya kila linalowezekana hata Kama huwezi ingia maombi ya masaa 12 kila siku kwa siku tatu omba Mungu Ategue kila aina ya mitego yakimapepo iliyopangwa juu yako (kwakua imeandikwa Isaya : Mlango 54
      17 Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema BWANA.
      TATU> soma sana neno la Mungu maana lenyewe ni taa ya maisha yako na hukuoonya na kila hali ukilifahamu na kuliweka kwa wingi kwako pia usiache kuomba sana.

      Delete
  15. Shalom.
    Nimeota mwanàngu wa Kwanza Amelia kichaa ghafla naomba maana yake

    ReplyDelete
  16. Bwana yesu asifiwe yani usiku wangu ulikua mgumu Sana leo ..kwanza nmeota nipo Arusha kwenye shule ya Laizer nmeenda kutembea ghafla nikaanza kuona nyoka wakawa wananikimbiza ..nyoka wa pili nikamkuta kwa marehemu babu yangu nyumban kanikimbiza mwisho wa siku akapanda juu ya Dali ...sjakaa sawa mwingne huyo nikastuka nkasali na kubatilisha ndoto .ndo kuanza kugoogle maana za ndoto ..naomba nisaidie hii Inamaana gan .cz Niko na woga

    ReplyDelete
    Replies
    1. Habar Mtumishi kwa roho vamizi iliyokukumba. Hii Ni Nguvu ya upinzani kwakila utakalofanya na kuua ulivyonavyo hukupaswa kuanza ku-google maana za ndoto kwanza ulipaswa kukemea kwanguvu maana ni shetani ametumia ajenti wake mwenye uwezo wa kuku-atack hivyo hujachelewa ingia maombi kwa siku tatu kufufua kila alichofanikiwa kuua katika ulimwengu wa roho kisha jitahidi sana kuwa na maombi kwakila utakalolifanya Mungu alifunike kwa damu ya Yesu.

      Delete
  17. Shalom nmeota namuuwa mtu ambaye simfahamu kwa kisu nikamchinja kabisa na nilikuwa nauwa mbele ya ndugu zangu na wao wananisaport kabisa
    Hii inamaanisha nini!?

    ReplyDelete
  18. Shalom nmeota namuuwa mtu ambaye simfahamu kwa kisu nikamchinja kabisa na nilikuwa nauwa mbele ya ndugu zangu na wao wananisaport kabisa
    Hii inamaanisha nini!?

    ReplyDelete
  19. Je ukiwa unamuota mtu mmoja tu kwa matukio tofauti, yaani hata kama wapo wengi lakini lazima na yeye yupo au wakati mwingine anakuwa peke yake..
    Hii ina maana gani?

    ReplyDelete
    Replies
    1. mmcgumva wangu nn ananiambia toka nimeenda kwao kumchumbia, anaota ndoto lkn
      hamuoni sura,. na hua inajirudia hta mchana,. maana yake nini?

      Delete
    2. mchumba wangu
      ananiambia toka nimeenda kwao kumchumbia, anaota ndoto lkn
      hamuoni sura,. na hua inajirudia hta mchana,. maana yake nini?

      Delete
    3. Umeokoka!? Ingia kwenye maombi Kunakitu mungu anataka asawazishe kwenye maisha yako jitahidi sana sana. Maana KUNA MAISHA AMBAYO YATAKUOATA YATAABU SANA USIPOMTAKA MUNGU SASAIVI UKIINGIA KWENYE NDOA BILA KUMTAKA MUNGU UTAHANGAIKA MNOOOO NA NDOA. mshirikishe maombi muingie pamoja maana nimaisha yenu wote.

      Delete
  20. habari...mimi nimeota nimelala lakini naona mtu kavaa nguo nyeusi anasogea kitandani(zaidi ya mara 2 naota hivi) na namuona kuanzia kiunoni kushuka chini.....nikiwa usingizini hivohivo uwa nakemea na kusali sana afu nashtuka kama nilikua naota huku bado nakemea.....hata jana usiku imejirudia......je inamaana gani?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Huyo ni adui wa karibu Yako Sana asiyetaka umjue, lakini anatumiwa na nguvu ya Giza ndio like vazi jeusi uliloliona, unachotakiwa kufanya nitakuombea na kisha utaingia Katika maombi ya siku mbili masaa kumina mbili Kila siku mwambie Bwana akupiganie vita hizi sio Kwa NGUVU zetu tunashinda ila Kwa msaada mkubwa was NGUVU za Mungu aliye hai 0767769942

      Delete
  21. Habari...mi nimjamzito sasa nimeota eti nmejifungulia nje ya hospitali mtoto mwenye jicho moja na macho mengine yapo miguuni afu mtoto yule akachukuliwa na mama mweupe ambaye simfahamu akidai kua yule mtoto ni wakwao...naomba uniambie maana yake

    ReplyDelete
    Replies
    1. Dada Ni serious case hii umekwisha jifungua!? Kama bado nitafute 0767769942.

      Delete
  22. Habari...mimi ninamwenza wangu na mara nyingi anaota ndoto anazaliwa tena na mtu tofauti na mama yake lakini pia ndoto hiyo hiyo kaiota tena na leo na kajiota yeye na mimi wote kwa pamoja tunazaliwa tofauti yeye kama kawaida huyo mtu anaemzaa hamjui ila huyu alie nizaa mimi anasema kama anamfahamu sasa naweza pata tafsiri ya hii ndoto tafadhari......

    ReplyDelete
  23. Ni Nani wako huyo mwenzio!? Mmeokoka!?

    ReplyDelete
  24. SHALOM MIMI NIMEOTA TB JOSHUA KAJA ALAFU KASHUKIA KWA JIRANI YANGU NIKAWA NAUMIA SANA KATIKA NDOTO KWANINI HAJI KWANGU WAKATI MIMI NDIE NILIKUA NA WASILIANA NAE SANA NA ALINIPENDA NA KWAHUYO JIRANI YANGU NI DADA YANGU WAKAKAA WAKAONGEA WAKAMALIZA WAKATOKA BILA KUNISEMESHA KABISA NILIHUZUNIKA SANA ALIPOONDOKA NIKAWA KARIBU NADADA ILI ANIAMBIE ALICHOAMBIWA LAKINI HAKUNIAMBIA BADALA YAKE AKAWA ANAONGEA VITU VINGINE KABISA NAOMBA MSAADA WAKO NIMEOKOKA NAMPENDA SANA YESU

    ReplyDelete
    Replies
    1. AMINA. SASA BASI TAFSIRI YA NDOTO HII NIKWAMBA...., Mungu ameandaa majibu ya mahitajibyako kwa mtumishi wa mungu unayedhani hawez kukusaidia... Amekuonyesha msaada hautoki mbali hata ungetumia gharama Mungu amekuandalia hapo uliponkwa mtumish huyo wa mungu aliye mwamini. JAMBO LAKUFANYA ingia kwenye maombi mwombe Mungu kupitia Bwana wetu Yesu kristo toba hasa, toba kwamba hukujua yakupasayokutenda nakuona kanakwamba Mungu anapatikana toka mbali, KISHA Mungu atafunua majibu yako kupitia mtumishi huyo wa karibu na kukusaidia KIKAMILIFU sana. Ubarikiwe.

      Delete
  25. Bwana yesu asifiwe nimeota ndoto kuna mtoto kanifuata kaniomba nimnunulie viatu vya shule sasa sielewi maana ya hiyo ndoto na inanijia kila dakika

    ReplyDelete
    Replies
    1. AMINA... Tafsiri yake nikwamba.... MUNGU AMEKUAMINI KUWA NI MTU UTAKAYEKUA KARIBU ZAIDI NA MTUMISHI WA MUNGU (kama Ni binti basi ww ni mama mchungaji na kama nikijana basi ww ni msaada mkubwa kwa mchungaji wako... Haijalishi ukokwenyewakati gani Mungu yuko kwenye matengenezo kwaajiliyako. JAMBO LA KUFANYA mshirikishe Mungu maana yeye ndo mwenye wazo lake ishi sana katika maombi na kumuhitaji roho mtakatifu kukuongoza kila wakati. UBARIKIWE.

      Delete
    2. TAHADHARI! inawezekana ukawa si mama m hungaji lakin msaada kwa mtumishi wa Mungu (nieleweke hilo)

      Delete
  26. Bwana yesu asifiwe,Mtumishi wa bwana,mara kadhaa huwa naota ndoto nipo na watu ambao walikwisha fariki siku nyingi hasa ndugu zangu,tafsiri yake no nini?

    ReplyDelete
  27. Bwana yesu asifiwe,kila Mara naota nipo chooni au nateleza nakaribia kuanguka chooni na mda mwingine naona kinyesi cha mtu naomba msaada maana hii ndoto inanitesa sana

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hii Huwa ni karibu na kuingia jaribu zito, shetani ameandaa mtego juu yako umefanya vizuri kunishirikisha nitakubeba pia Katika maombi ila ww binafsi ingia maombi na mwambie Mungu akupe uvumilivu na namna ya kutoka Katika mazito hayo.

      Delete
  28. Nimeota ndoto Kuna kitu ambacho nilikifahamu nilipoanza safari ya kutembea kukifuata mahali, lakini njiani miguu ilikuwa inaishiwa nguvu, na Kuna mahali mtu akanipa ushauri wa kubadilisha Mafuta ninayotumia kupikia Chakula, nikaendelea na safari kwa kujilazimisha Hadi nikafika eneo lenyewe lakini nikasahau nilichokifuata. Ina maana gani mtumishi?

    ReplyDelete
  29. Bwana Yesuasifiwe ukiota unamwona farasfi anatekimbia Sana inatafsiri gani

    ReplyDelete
  30. Nimeota naombewa na mtumishi mkubwa wa Mungu na nikaamka bado naweweseka

    ReplyDelete
  31. Bwana yesu asifiwe, leo nimeota naokota pesa Kuna nyumba ya jiran karibu na ninapofanyia biashara nmeota not za elfu 10 na elfu 5 nmeokota nyingi , nikirud ofisin mwenye nyumba wangu alikua ananidai 30 nikampa na ndiz na io pesa Ambayo nyingne nmeokota nikaweka pamoja na ndiz za kupika nikampa bas nitafurah ni nn maana yake? Pia hua naota najiandaa kufanya mtian niko bize sana kujisomea hizo Dakika za mwisho watu wanapokua wanaulizana mm nikisikia nakisoma hicho kitu faster faster ila sijawah fanya huo mtian ila naotaga tu najiandaa na zimebak Dakika chache mtian uanze. ..ni nn maana yake ?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Bwana Yesu asifiwe wapendwa .mimi sijaenda shuleni nilikuwa nachunga kwa mda mrefu.lakini baadae nikaja mjini ila kila siku naota nikichunga ng'ombe.jamani maana yake ni nini

      Delete
    2. Nitafute kaka nikusaidie Ili ufanikiwe mjini, maana wale ulio waacha wamekushikilia bado na ndio maana hali huja ya kuchunga lazima ujiondoe Rohoni na hali za kuchunga la sivyo vyote utakavyo fanya mjini havifanikiwi.

      Delete
  32. Hata wakati mwingine ninaota baba yangu alinilisha nyama baada yakula akasema kimbia kazirudishe ng'ombe maana yake nini

    ReplyDelete
  33. Habari, naomba nisaidie tafsiri ya ndoto ambazo nimekua nmeota mfululizo kwa siku tofaut tofaut, hizi ndoto zinakua kwa namna nakemea nguvu za giza au wakat mwingine kiumbe mwenye mfano wa binadamu nisie weza kuona au kujua sura! mara nyingi hua najikuta nikikemea na kuomba kwa nguvu nakua siwezi kufany chochote kuinuka wala kufumbua macho lakin nikipamban kufumbua nimuone mtu najikuta nashtuka na kuamka.

    ReplyDelete
  34. Habari,naomba nisaidiwe tafsiri ya ndoto nilizo ota kwa wakati tofauti? ,1.niliota nafunga ndoa na mwanamke nisie mfahamu jina lakini kisura namfahamu kuwa ni mwigizaji wa filamu za kibongo ila watu walio kuwa wakinifungisha ndoa iyo siwafahamau kabisa?
    2.niliota na fanya tendo la ubakaji kwa mtoto wakike wa kaka yangu,na kwa mazingira nisio yaelewa kabla sijafanikiwa kufanya mahafa ayo nikajikuta nipo mezani ofisini na mimi nikiwa ndo bosi nikizungukwa na watu nisio wajua kisha pembeni mwa meza iyo palikuepo na familia yangu yani watoto wangu 3 na mkewangu wakipata kifungua kinywa lakini jambo lakushangaza nilimpiga mkewangu kofizito sana mbele ya watu walio kuwa mezani na kisha nika mwomba msamaha papo hapo

    ReplyDelete
    Replies
    1. Pole Sana AISEE sikupitia blog muda mrefu Sasa, na Ndo to Hz zinatakiwa uzielewe Sanna haraka,nitafute 0767769942

      Delete

Post a Comment

Popular posts from this blog

UCHAWI KIUHALISIA

UHALISIA ROHONI