ULIMWENGU WA MAPEPO
src="https://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js?client=ca-pub-5030735873453842"
crossorigin="anonymous"></script>
UONGO UNAO ENEZWA NA MAPEPO

Inaendelea......
Wakati huo nikiwa katika mkutano huo wa kimapepo, Katika hotubayake "Elam (pepo kiongozi mkuu katika ngazi ya shira)" alituambia kua jina la siri la Yesu lilikua ni Yesu Ajonichim, na akanukuu katika biblia maneno yaliyo andikwa "Nae anajina lililo andikwa asilolijua mtu ila yeye mwenyewe"(Ufunuo 19:12) Alidai kuwa Ajonichim ni jina la siri la nafsi ya pili ya Yesu, alilopewa wakati akitunukiwa ngazi ya pili ya kipepo inayojulikana kwa jina la Kal 666 na kwamba kiongozi wake wa kiroho alikua Zadok.
Elam alitujulisha kua hadi leo YESU anaendelea kuteseka huko Kosa (kosa ni gereza la kipepo ambalo lipo huko Retz) alisema amkosa hayo ni adhabu ya yeye kufanya makosa alipokua duniani kama binadamu. Elam alitoa mfano kua, Yesu alikua amefikia ngazi ya pili ya vyeo vya nguvu za giza, lakini alivunja viapo kwa kufanya kinyume na maagizo ya kiongozi wake Zadok, na akaanza kufanya miujiza mbalimbali huko duniani bila ruhusa ya viongozi wa nguvu za giza. Elam akaendelea kusema kutokana na makosa hayo makubwa na mengine mengi madogomadogo, Zadok akawa na uwezo wa kumuondolea Yesu uwezo wa kufanya miujiza, kiasi kwamba wakati wa kufakwake msalabani akalia akisema "Mungu wangu wa Zadok na roho zote za Herosi mbona umeniacha?"

Elam akaendelea kusema huku akisisitiza vikali kua Wafuasi wote wa Yesu kristo ni waalifu ambao wanatafutwa vikali ili kuahdibiwa na Mungu, kwa mujibu wa Elamu anasema wakristo hao wanajaribu kutumia maombi usiku na mchana ili kutaka kumtoa yesu kifungoni. Elam alisisitiza na kusema kua nijukumu letu sote wenye nguvu za juu, kufanya kazi kama police wa juu kuwakamata Wakristo hao na kuwaleta mbele ya Mungu Naga, ambate ndiye Mungu wa kifo na adhabu kwa wanadamu
Elam akaendelea kusema hiyo adhabu dhidi ya wakristo isingeendelea kuwepo endapo tu wangekubali na kuacha kuomba pia kuamini kwamba Yesu atatolewa pale tu atakapo maliza kutumikia adhabuyake .Akasisitiza tena akasema na wakristo kuamini kua YESU alikufa kwaajili ya dhambi za wanadamu nikosa lingine kubwa sana, kwasababu YESU hakufa kwaajili ya dhambi ya mtu yeyote ispokua dhambizake mwenyewe.
Pia katika mkutano huo pia Elam alituambia ninini sala za waumini wa KRISTO YESU kutoa moshi katika ulimwengu wa roho, alisema kua moshi ulitokana na ukweli wa sala kama hizo hazikuweza kutimiza malengoyake ya kumfungua Yesu kutoka kifungoni, hivyo zilibadilika na kua moshi na kuharibu kazi zingine za nguvu za giza katika ulimwengu wa roho. MTUMISHI WA MUNGU(kwasasa ambaye amemkataa shetani na kazi zake zote) IYEKE NATHAN UZORMA anasema "ukweli ni kua hotuba ya Elam ilinifanya niamini (kwasababu imani huja kwa kusikia) na kuanza kupambana kwa kasi na ari mpya dhidi ya wakristo kwakudhani kua kwawakatiule nilikua nnafanya kazi nzuri ya kumpendeza mungu na mtu. IMEANDIKWA katika Yohana 16:2-3 2Watawatenga na masinagogi; naam, saa inakuja kila mtu awauaye atakapodhania ya kuwa anamfanyia Mungu ibada. 3 Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi.

Ni ukweli usiopingika kabisa Shetani Ibilisi ambae ni baba wa uongo yuko kazini vikali kupigana katika ulimwengu wa Roho edha uwe unajua au hujui au unapigana katika ulimwengu wa roho au umebweteka ukweli ni huu kwamba vita ya Shetani juu ya WAKRISTO TULIOOKOKA ni kali sana katika ulimwengu wa Roho na SIO kuokoka tu ukisha jitangaza wewe ni MKRISTO shetani anapambana vikali na wewe tena kwa njaa yakukuua kabisa hivyo sio muda wakuupoteza hali haupo katika maombi na kuzivaa kikamilifu zile silaa za imani hii ya BWANA NA MWOKOZI WETU YESUKRISTO.
<script async src="https://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js?client=ca-pub-5030735873453842"
crossorigin="anonymous"></script>
<script async
thaks mtumishi wa bwana
ReplyDelete