Posts

KURUDI KWA YESU MARA YA PILI SEHEMU YA KWANZA

KURUDI KWA YESU MARA YA PILI SEHEMU YA KWANZA       Ujio wa Yesu kwa mara ya kwanza kama kulivyotabiriwa kulikamilika kwa kupitia kuzaliwa na bikira Mariamu. Aliishi kwa makusudi maalumu ya kuleta ukombozi kwa njia ya kifo pale msalabani (Marko 10:45). Wakati maisha na huduma yake hasa wiki ya mwisho aliongea habari za kuondoka lakini kwamba angerudi tena (Yohana 14:1-4; Mathayo 24:4-31). Baada ya kumaliza kazi hiyo msalabani alipaa na kwenda kwa Mungu Baba na malaika waliwakumbusha wanafunzi wake kwamba huyo Yesu waliyemwona anapaa atarudi tena (Matendo 1:11).   Kurudi kwa Yesu ni fundisho la msingi la imani ya kikristo ambalo ni tumaini lenye baraka. Fundisho hili huleta hamasa na shauku ya kumngoja Yesu kwa hofu na utakatifu hali tukimtumikia Mungu kwa juhudi kwa sababu ushirika wa sasa na Kristo una uhusiano na matokeo makubwa sana katika maisha yajayo ya milele. Kuja kwa Yesu mara ya pili  vi | F a h a m u K u h u s u K U R U D I K W A Y E S U  ...

AINA TATU ZA MAUTI

AINA TATU ZA MAUTI NA NGUVU ILIYOMO NDANI YA HIYO AINA YA MAUTI. Mauti hasa ni Nini? U-Mauti ni Kifo. MAUTI ni hali au kitendo cha mtu kutoka katika uhai kuingia KIFO/KUFA (Mfano wa msemo; Umauti ulimkuta akiwa safarini kuja hapa! (ni kitendo). U-mauti unapo mjia mtu huwa anashindana nao pasipo kujua ki-mwili, wengine huaga wapendwa wao Kwa hali kanakwamba ni fumbo asilolijua hata muagaji anaye aga. KIFO/KUFA ni kutokua na mawasiliano kabisa kati ya mwili na roho, yaani ni hali ya milango ya fahamu kutofanya kazi tena kabisa na kuanza kuharibika, moyo kushindwa kuendelea na kazi yake ya kusukuma damu hivyo mwilini damu huganda na hapo ndipo ulipo mwisho wa uzima wa mwili huu. ( wakati huo roho ya mwanadamu huendelea kuishi ) AINA ZA MAUTI 1.MAUTI YA KWANZA. >Huua mwili (Mwili kuachana na Roho) 2.MAUTI YA PILI. > Roho kuhukumiwa adhabu ya moto. 3.MAUTI YA TATU. >Mtu anaishi/anapumua, ila hampendezi Mungu. somo Lina endeleaaa.........

AINA TATU ZA MAUTI

AINA TATU ZA MAUTI NA NGUVU ILIYOMO NDANI YA HIYO AINA YA MAUTI. Mauti hasa ni Nini? Mauti ni mwili ulio KUFA. MAUTI ni hali au kitendo cha mtu kutoka katika uhai kuingia KIFO/KUFA (Mfano wa msemo; Umauti ulimkuta akiwa safarini kuja hapa! (ni kitendo). U-mauti unapo mjia mtu huwa anashindana nao pasipo kujua ki-mwili, wengine huaga wapendwa wao Kwa hali kanakwamba ni fumbo asilolijua hata muagaji anaye aga. KIFO/KUFA ni kutokua na mawasiliano kabisa kati ya mwili na roho, yaani ni hali ya milango ya fahamu kutofanya kazi tena kabisa na kuanza kuharibika. AINA TATU ZA MAUTI

NABII NI NANI KI-BIBLIA?

 JINSI YA KUWATAMBUA MANABII WA KWELI. Katika somo hili nitaelezea jinsi ya kuwatambua manabii wa kweli wa Mungu kutokana na sifa walizokuwa nazo wakati wa Agano la Kale na Agano Jipya. Ni muhimu kila mkristo aliyeokoka aweze kupambanua (kutofautisha) na kutambua manabii wa kweli na manabii wa uongo. Manabii wa kweli walikuwa na sifa zifuatazo; 1.Walikuwa waaminifu. Hapa tutaangalia manabii watatu ambao ni Yesu, Musa na Samweli ambao walikuwa waaminifu katika mambo yote ya Mungu. Waebrania 3:1-2 “...Yesu aliyekuwa mwaminifu kwake yeye aliyemweka, kama naye Musa alivyokuwa, katika nyumba yote ya Mungu.” Katika andiko hili, Yesu amefananishwa na nabii Musa alivyokuwa mwaminifu. Mwingine ni Samweli, alipokuwa mzee aliwashuhudia wana wa Israel jinsi alivyokuwa mwaminifu tangu akiwa kijana. 1Samweli 12:2-4 “Basi sasa, angalieni, mfalme anakwenda mbele yenu; na mimi ni mzee, mwenye mvi; tena, tazameni, wana wangu wapo pamoja nanyi; nami nimekwenda mbele yenu toka ujana wangu hata ...

MAOMBI USHTUKAPO NDOTONI

 MAOMBI USHTUKAPO NDOTONI (NDOTO MAJIBU) Unapo-amka usingizini sikuzako zote, usingizi wa ndoto yaani mfurulizo wa matukio wakati umelala kitandani/popote ulipo sinzia, kwanza usinung'unike mbele za Mungu kana kwamba Mungu hakupendi wewe, au ameruhusu ndoto ya namna hiyo ikupate kwanini hilo litokee kwako. Maandiko husema, Ayubu 33 (Biblia Takatifu) ¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯ ¹⁴ Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. ¹⁵ Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani; ¹⁶ Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao, Pia neno linazidi kueleza Ninini kusudi la ndoto husika, Ayubu 36 (Biblia Takatifu) ¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯ ⁹ Ndipo huwaonyesha matendo yao, Na makosa yao, ya kuwa wametenda kwa kujivuna. ¹⁰ Yeye huyafunua masikio yao, wasikie maonyo, Na kuwaagiza warudi kuuacha uovu. ¹¹ Kama wakisikia na kumtumikia, Watapisha siku zao katika kufanikiwa, Na miaka yao katika furaha. ¹² Lakini wasiposikia, wat...

NDOTO YANGU

Napata taabu Sana, ndoto yangu niliyoota imenifanya nimekosa raha,nimekosa usingizi,nimekosa hamu ya kula ninatokwa na machozi pekee sina raha Wala amani. Je! Nikweli umekosa amani kwaajili ya ndoto!? Je! Tangu uote ndoto hiyo uliyowahi kuota maisha yamebadirika!? Je! Unaona uadui tangu uote ndoto hiyo? Je! Ni kweli ndoto ile itakua chanzo cha umasikiniwangu!? Je! Kuanguka kiuchumi hivi chanzo ni ile ndoto!? Je! Kifo kile chanzo ni ile ndoto kweli? Je! Mafarakano haya chanzo ni njozi ile!? Je! Nini kimefanya nilie usingizi!? Je! Kuna nini, kuota waliokufa!?  Nimekosa nini niote ndoto mbaya Mimi kila siku!? Ndoto hizi kwanini zinanipa majuto kila siku!? Oooooooooooooh! Kumbe ndoto zinamapana makubwa mnoooo kila mmoja huota ndoto, japo wapo kadhaa wasioota ndoto lakin kunajambo linakua haliko sawa Sana.    Ayubu 33 (Biblia Takatifu) ¹⁴ Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. ¹⁵ Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwaji...

NAMNA YA FANYA MAAMUZI YA HEKIMA HASA UKIWA KIJANA.

Image
 NAMNA YA FANYA MAAMUZI YA HEKIMA HASA UKIWA KIJANA (somo na Mwl.Christian Myeya) Joshua 24:15. 15. And if it seem evil unto you to serve the LORD, choose you this day whom ye will serve; whether the gods which your fathers served that were on the other side of the flood, or the gods of the Amorites, in whose land ye dwell: but as for me and my house, we will serve the LORD. Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia BWANA, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia BWANA.       NINA KUOMBEA KWA MUNGU BABA KUPITIA BWANA NA MWOKOZI WETU YESU KRISTO ALIYE HAI UWEZE KUYAELEWA YOTE KWA MAPANA MAKUBWA YA ROHO MTAKATIFU USOMAPO SOMA HILI AMINA. Basi atika  somo letu hili ili kuweza kueleweka kirahisi zaidi nianze na kutoa maana za maneno yaliyoko katika kichwa cha somo hili:- MANENO HAYO YALIYO UNDA SOMO N...